Tumbo kujaa gesi, mwili kuwa mnene, uchovu wa mwili, kujisikia vibaya, mwili kutokwa na jasho ni baadhi ya dalili nyingi za homoni imbalansi kwa wanwake. Vipindi vya hedhi kuruka au kuchelewa vinaweza pia kusababishwa na homoni imbalansi. Uwiano huu unaweza kuathiri afya, utendaji wa kazi, mahusiano ya ndoa pamoja na faraja ya moyo wa muhusika. Dalili za homoni imbalansi kwa wanawake ni kama hizi zifuatazo:
• Kutokwa na jasho wakati wa usiku
• Kukosa hamu ya tendo la ndoa
• Kutokushika ujauzito
• Kuhisi kichefuchefu
• Kukosa usingizi
• Kuwa na huzuni
• Kukosa hamu ya kula
• Kichwa kuuma
• Uzito kuwa mkubwa au
• Uzito kupungua
• Kuwa na harara kwenye ngozi
• Mifupa kudhoofika
• Nywele kuwa nyembamba
• Nywele kunyonyoka
• Mabadiriko ya sukari kwenye damu
• Kuhisi kiu
• Matatizo ya macho
• Kisimi cha uke kuwa kikubwa
• Kuhisi uchovu sana