Mwani (Sea Moss) ni mmea wa baharini wenye virutubisho vingi vinavyoweza kusaidia mwili kufanya kazi vizuri.
Faida za Mwani Kitaalamu
• Chanzo kizuri cha madini ya potasiamu, ambayo husaidia udhibiti wa shinikizo la damu.
• Hulainisha mfumo wa chakula, kusaidia mmeng’enyo, kusafisha utumbo na kupunguza muwasho wa tumbo.
• Zipo tafiti zinazoonyesha kuwa kiungo cha fucoxanthin kinaweza kusaidia katika udhibiti wa sukari mwilini.
• Mwani una magnesium, madini ambayo mara nyingi huwa kidogo kwenye vyakula vya kawaida.
• Una zinc, madini yanayochangia afya ya mfumo wa uzazi na nguvu za mwili.
• Una nyuzi (fiber) zinazosaidia kushiba haraka na kupunguza ulaji wa kalori – muhimu kwa kudhibiti uzito.
• Una calcium, inayosaidia afya ya mifupa na viungo.
• Ni chakula cha alkaline, hivyo kinaweza kusaidia uwiano wa asidi mwilini.