Siku zote ukisikia miguu inawaka moto fikiria nyanya za umeme wa mwili zinazopeleka umeme kwenye miguu. Hizi nyanya tunaziita neva za fahamu. Kama hizi nyanya zikipata shida (peripheral neuropathy) unasikia maumivu kama kuwaka moto kwenye miguu.
Kuna vyanzo vingi vinavyosababisha shida hii. Angalia hapa na gundua ambayo inaweza kuwa inakuhusu
1. KUCHOKA
Hii huwapata wale ambao wanafanya kazi ya kutembea muda mrefu, kusimama muda mrefu au kukaa muda mrefu.
2. KISUKARI
Sukari nyingi kwenye damu inapelekea kuharibu mishipa ya damu inayozilisha neva za fahamu za miguuni na hivyo hizi nyanya zinaharibika.
Wakati mwingine kama unashida ya miguu kuwaka moto bila sababu maalumu na isiyosikia matibabu, kapime sukari.