NIPIGIE SIMU, NITUMIE SMS AU NITAFUTE WHATSAPP ILI TUWASILIANE KWA UKARIBU ZAIDI USIOGOPE KUNITAFUTA
Open
• Jumatatu - Jumapili, 00:00-23:59
Je... , unafahamu kwa ufupi sababu, madhara, kinga na tiba ya kusaidia kuondokana na mafuta mabaya kwenye mishipa ya damu (bad cholestrol)?
cholestrol ni nini?
cholesterol ni mafuta ambayo hupatikana katika damu. mwili unahitaji cholesterol kujenga seli zenye afya, lakini kiwango cha juu cha cholesterol hubadilika na kuwa mafuta mabaya (bad cholestrol). kiwango hiki kikubwa kinaweza kusababisha magonjwa ya moyo.
na kiwango kikubwa cha mafuta haya kwenye damu hujikusanya kwenye mishipa ya damu na hivyo kupelekea damu kutoweza kupita vema. hapa tuone mfano hai kabisa wa bomba la maji linalotoa maji kwa presha halafu ukaliziba mara moja na kuona jinsi maji yanavyoongezeka presha, ndivyo vivyo hivyo hutokea pia kwenye mishipa ya damu inayopitisha damu kwenda katika sehemu mbali mbali za mwili kutoka kwenye moyo.