Wafugaji wenzio wanafanikiwa kwasababu kubwa moja nayo ni " wanaongeza thamani katika ufugaji wao kwa kufuata kanuni na taratibu sahihi za ufugaji"
hiki ni kitendo cha kuondoa/kukata sehemu ya ncha ya mbele kwenye upande wa juu na chini wa mdomo wa kuku.
mdomo wa kuku una asili ya ncha ambayo inaweza kukatwa kiasi kupunguza ncha yenye madhara ya kutoboa, kurarua na kujeruhi, na kuku akaendelea na maisha kama kawaida.
kukata mdomo kwa kuku kumelenga kumfanya kuku asijeruhi wenzake au kutoboa mayai na kuyala.
kuku waliokatwa midomo, midomo yao hubaki butu, hivyo hawawezi kutoboana au kula mayai.
kuku wasipokatwa midomo ni jambo la kawaida kuona wakimshambulia mwenzao kwa kumtoboa toboa vidonda hadi kufa.
kanuni za debeaking/ukataji mdomo wa kuku
umri mzuri kukata midomo ya kuku ni miezi miwili hadi mitatu ya umri wao.