SIRI 7 ZA KUPONYA MOYO ULIOVUNJIKA BAADA YA USALITI NDANI YA NDOA
UTANGULIZI
Usaliti ndani ya ndoa ni moja ya maumivu makali Zaidi ambayo mwanadamu unaweza kuyapitia.Unagusa kiini cha uaminifu wako ,unatikisa misingi ya maisha yako , na kukuacha ukiwa na maswali mengi yasiyo na majibu. Ni hisdia inayoweza kukufanya uijihisi mpweke, uliyepoteza mwelekeo na mnyonge.
Hata hivyo, dhumuni la kitabu hiki sio kukuambia kuwa maumivu yako sio kitu. bBadala yake, kipo hapa kukuhakikishia kuwa maumivu hayo sio mwisho wako. Kitabu hiki ni mwongozo wa vitendo ulioundwa kukusaidia kupita kwenye bonde hilo la gizandani ya siku 7. Kupitia siri hizi rahisi lakini zenye nguvu za kisaikolojia na kiroho,utajifunza jinsi ya kuachia mzigo wa hasira, kuzuia mawazo yanayokutesa usiku, na kurejesha hadhi na thamani yako uliyozaliwa nayo.