Kisababishi kikuu cha saratani ya mapafu ni
1. kuathiriwa na moshi wa tumbaku
unaosababisha asilimia 80–90 ya saratani. Wasiovuta huchangia visa hivi kwa asilimia 10-15–
[3] na mara nyingi huhusishwa na muungano wa masuala ya kijenetiki,
[4] gesi ya viwandani,
na uchafuzi wa hewa, pamoja na moshi kutoka kwa anayevuta sigara.
Matibabu na matokeo ya muda mrefu hulingana na aina ya saratani, hatua (kiwango cha uenezi), na afya kwa jumla ya mtu, ikipimwa kwa hali ya utendakazi.
Matibabu ya kawaida ni pamoja na upasuaji, kemotherapi, na radiotherapi. KMSK wakati mwingine hutibiwa na upasuaji, ilhali KMSN huwa bora kwa kemotherapi na radiotherapi.
Ulimwenguni kote, saratani ya mapafu ni kisababishi cha kawaida cha vifo vinavyohusiana na saratani kwa wanaume na wanawake, na husababisha Vifo milioni 2.0 kila mwaka.