Hii ni system ya kutambua uvamizi au uwepo wa watu kwenye eneo ndani ya muda usio tarajiwa.
System hii ina PIR sensor (passive infrared sensor), window and door sensor, control panel, panic button pamoja na king'ora ambavyo kwa pamoja huikamilisha.
System hii ina sensor mbili tofauti Ambazo ni PIR kwaajili ya kutambua movement na window or door sensor kwaajili ya kutambua dirisha au mlango uliofunguliwa/uliovunjwa.
System hii hutumia line ya simu ambayo itaunganishwa na simu za watu mpaka 5 kwaajili ya kutoa taarifa kwa njia ya SMS pia itaweza kupiga simu kwenye namba tano kati ya hizo kuwapa taarifa ya uvamizi.
Katika kudetect uvamizi system hii hutoa tahadhari kwa mvamizi kwa kupiga king'ora, ambacho pia husaidia kwa watu walioko karibu kuchukulia hatua ya uvamizi huo.
Umuhimu wa hii system ni mkubwa na itaweza kukuepusha na mengi ikiwa si kwa wavamizi tu, hata wanafamilia unaweza kucontrol ni wapi wasifike, kuimarisha mipaka yako na kukupa amani ya faragha yako.